• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

Halmashauri ya Mji Njombe kukusanya bilioni 4.1 kupitia mapato ya ndani mwaka 2020/2021

Tarehe iliyowekwa: January 20th, 2020

Baraza  la Waheshimiwa Madiwani Halmashauri ya Mji Njombe limepitisha bajeti yenye thamani ya Shilingi Bilioni 4.1 kwa mwaka wa fedha 2020/2021 kutoka Bilioni 3 kwa mwaka wa fedha 2019/2020, ongezeko litokanalo na  ukamilishaji wa miundombinu ya ujenzi wa stendi kuu ya mabasi, upanuzi wa masoko ya mbao na ujenzi wa  soko kuu.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa Baraza la bajeti Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Njombe Edwin Mwanzinga alisema kuwa kwa mwaka wa fedha 2019/2020, Halmashauri imeendelea kufanya vizuri katika sekta mbalimbali ikiwemo Elimu, Afya, Usafi wa Mazingira, Ujenzi, ukusanyaji mapato na yote ni kutokana na ushirikiano uliopo kati ya Madiwani na Wataalamu katika kusimamia utekelezaji wa miradi hiyo.

“Katika mwaka wa fedha ujao inabidi tukubaliane kuwa wakati wa kazi ni kazi haitakiwi kuoneana aibu. Sisi wanasiasa ndio tunaiangusha Serikali yetu wenyewe kutokana na kauli zetu na kutosimamia ukusanyaji wa mapato ipasavyo kwa hofu ya kutopigiwa kura. Bora kukosa kura lakini tukusanye mapato tukumbuke kuwa Wanachi ambao ndio wapiga kura hawatatupigia kura kama maendeleo yasipokuwepo” Alisema Mwanzinga.

Akiwasilisha rasimu ya mpango wa bajeti ya makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka wa fedha 2020-2021, Kaimu Mchumi wa Halmashauri Emma Lunojo alisema kuwa ongezeko la wigo wa mapato ya ndani litaipa Halmashauri uwezo wa kuendelea  kuwekeza kwenye miradi mingine yenye kuongeza vyanzo vya mapato kwa Halmashauri na huduma kwa Wananchi ambapo jumla ya shilingi bilioni 2.5 kutoka mapato ya ndani zinatarajiwa kutumika kutekeleza miradi ya maendeleo.

Aidha, amefafanua kuwa kipaumbele cha Halmashauri kwenye bajeti ijayo ni kuendelea na kazi ya kukamilisha vituo vya afya vya Makowo, Kifanya, Luponde na Njombe Mjini vituo ambavyo vipo katika hatua mbalimbali za utekelezaji, uboreshaji wa huduma za elimu mapambano ya UKIMWI, udumavu/Lishe  na utoaji wa mikopo kwa vikundi vya uzalishaji mali.

Wakichangia katika nyakati tofauti juu ya makisio ya bajeti hiyo Abuu Mtamike Diwani wa Kata ya Mji Mwema, George Sanga Diwani wa Kata ya Ramadhani, Sigrada Mligo Diwani Viti Maalumu na Ultrick Msema Kata ya Luponde walisema kuwa kilio chao kikubwa ni kushuka kwa ukusanyaji wa mapato ya mbao kutokana na mgongano uliopo baina ya TRA Njombe wafanyabiashara wa mbao na Halmashauri juu ya ulipaji wa tozo za mbao na wameomba Mamlaka hizo kukutana na kupata muafaka wa mgogoro huo kwani kwa sasa kunaupotevu wa mapato uliosababishwa na mgogoro huo.

Kwa vipindi tofauti Halmashauri ya Mji Njombe imekuwa ikifanya vizuri katika ukusanyaji mapato kwa kukusanya kwa zaidi ya asilimia 100  na hivyo kuimarisha uwezo wa Halmashauri  kiuchumi na kuboresha utoaji huduma kwa manufaa ya Wananchi wote.



Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI,UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI. April 25, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA. December 20, 2024
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKUU WA WILAYA NJOMBE MHE. JUMA SWEDA ATOA WITO KUHUSU CHANJO YA PILI YA POLIO.

    April 29, 2025
  • AFISA MWANDIKISHAJI JIMBO LA NJOMBE MJINI AKUTANA NA VYAMA VYA SIASA

    April 24, 2025
  • ZIARA YA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA WILAYA YA NJOMBE KUKAGUA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    April 04, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Njombe awaonya wenyeviti kuhusu uharibifu wa miradi ya maendeleo

    February 15, 2025
  • Angalia zote

Video

WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI NA KUJITUMA
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe