Halmashauri ya Mji Njombe imefanikiwa kutoa mshindi wa Kwanza Kimkoa na wa tatu Kikanda katika kundi la Wakulima kwenye maonyesho ya nane nane mwaka 2019 ambapo Bi. Ajentina Mvile ameibuka kidedea na kujipatia fedha na cheti cha ushindi ambapo mgeni rasmi katika maonyesho hayo alikuwa Waziri Mkuu Mstaafu Mizengo Kayanza Peter Pinda.
Akizungumza mara baada ya kuibuka mshindi Bi Ajentina ambaye ni mkazi wa Kijiji cha Itulike Kata ya Ramadhan Halmashauri ya Mji Njombe amesema kuwa mambo yaliyompeleka kuweza kufanikiwa na Kuibuka Mkulima yeye akijikita kwenye zao la parachichi ni jitihada ambazo amekuwa akionesha katika kuzingatia mbinu za kilimo bora na chenye tija na kuhakikisha kuwa ushauri wa wataalamu wa kilimo unafanyiwa kazi.
“Kilimo kinahitaji jitihada binafsi. Tulipoanza kujishughulisha na kulima parachichi watu wengi waliona kama ni kupoteza muda. Hii ni kutokana na kuwa hapo mwanzo parachichi halikuwa na thamani na hali ya soko haikuwa ya uhakika.Wengi hawakuona Kilimo cha parachichi kama ni kilimo chenye tija.”Alisema Ajentina
Aliongezea kusema” Kwa sasa soko ni la uhakikika na mara baada ya kuona parachichi limepata soko nje na ndani ya nchi kila mtu sasa analima parachichi. Soko lipo na faida ipo. Nawashauri wakulima kuwa tunapopata taarifa ya kitu Fulani tusidharau kwani huwezi jua manufaa yake mbeleni.”
Kwa upande wake Waziri Mkuu Mstaafu wa awamu ya nne Mizengo Pinda akizungumza wakati wa kufunga maonyesho hayo na kukabidhi zawadi kwa Washindi amesisitiza jamii kuzingatia matumizi ya ulaji wa lishe bora ili kuwa na afya bora na kupamba na tatizo la utapiamlo ambapo kwa kiasi kikubwa mikoa ya nyanda za juu kusini ndio imekuwa yenye asilimia kubwa ya kiwango cha tatizo la utapiamlo.
“Kumekuwa na mabadiliko makubwa sana katika maonyesho haya haswa kwenye upande wa usindikaji.Ni vyema tukaona ni namna gani tunawawezesha wasindikaji hawa wadogo kupata alama ya ubora (TBS). Viwanda vione ni kwa namna gani vitatumia malighafi za wakulima na wafugaji. Alisema Pinda
Aidha amewataka wakulima na wafugaji kuongeza jitihada za zana za kilimo ikiwa ni matumizi ya mbolea,viuatilifu na maghala ya kuhifadhia chakula ikienda sambamba na utafuataji wa masoko ya ndani na nje.
Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.
Sanduku la Posta: S.L.P 577
Simu ya Mezani: 026-2968833
Simu ya Mkononi: 026-2968833
Barua Pepe: td@njombetc.go.tz
Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe