• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

Madiwani wakaguana na kukosoana Kwenye utekelezaji Miradi ya Maendeleo

Tarehe iliyowekwa: July 29th, 2021

Ni ziara ya Waheshimiwa Madiwani wa Halmashauri ya Mji Njombe iliyolenga katika kukagua, kujifunza na kutoa ushauri juu ya  miradi Mbalimbali inayoendelea katika Kata zao huku Madiwani hao wakipata wasaa kila mmoja kutembelea Kata ya mwenzake kwa kugawanywa katika kundi A na B na kufanya majumuisho kwa pamoja ambapo kila mmoja aliweza kuelezea alichojifunza na changamoto aliyobaini kwenye miradi iliyopo kwenye Kata aliyotembelea.

Katika ziara hiyo miradi mingi iliyotembelewa ni katika sekta ya Afya na Elimu ambapo Madiwani hao kwa pamoja wameweza kujadiliana na kupata  suluhu za Changamoto zilizoonekana katika miradi hiyo ili kuweza kuboresha na kuepuka makosa yanayoweza kujirudia huku Kata zilizofanikiwa kwa kuwa na miradi bora wakibadilishana uzoefu na maarifa kwa Kata nyingine.

Madiwani hao pia walisema kuwa licha ya kuwa jamii imekuwa ikichangia kwenye uanzishwaji wa miradi katika vijiji,mitaa na Kata bado mwamko wa Wananchi umekuwa ni mdogo jambo linalopelekea Halmashauri kuwa na mzigo mkubwa wa kupeleka fedha za miradi ya maendeleo na hivyo kuifanya Halmashauri kutoa kiasi kikubwa cha fedha za mapato ya ndani kukamilisha miradi hiyo jambo lililowafanya Madiwani kumpongeza Mkurugenzi na Wataalamu kwa kupeleka fedha hizo. Aidha Madiwani hao wamekubaliana kuendelea kuielimisha jamii na kuihamasisha jamii kuendelea kuchangia kwenye kufanikisha miradi hiyo badala ya kuitegemea Halmashauri pekee.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti tofauti katika kikao cha tathmini ya pamoja baada ya kutembelea miradi Madiwani hao wameonesha  kuridhishwa kwao na miradi mingi na kuendelea kumuombea Mkurugenzi wa Halmashauri aendelee kuwepo ili Yale yaliyosalia na aliyoanzisha mwenyewe aweze kumalizia. Waheshimiwa Madiwani wamesema kuwa yapo maeneo ambapo miradi imekua si ya kuridhisha kutokana na Aina ya mafundi ambao wamekua wakifanya Kazi za ujenzi jambo linalopelekea baadhi ya miradi kuwa chini ya kiwango.

"Ukiangalia katika miradi tuliyotembelea inatofautiana sehemu na sehemu.Kuna eneo katika Kata moja unakuta wamefanya vizuri sana.Lakini katika eneo jingine kwenye Kata hiyo hiyo ukakuta miradi yao ipo chini ya Kiwango.Kata ya Matola na Makowo tunafanikiwa kuwa na miradi bora kutokana na aina ya mafundi tunaowatumia.Hatuwatumii  mafundi wanaotoka katika eneo lenye Mradi(Mafundi wazawa).Ukiwatumia mafundi wazawa kila siku wanakuwa na sababu ya kutokuja kufanya kazi.Sisi tunawatumia mafundi kutoka Kata nyingine Mfano Lugenge wanakuja kufanya Kazi Matola na Makowo.Ndio maana sisi miradi yetu Haina shida."Alisema Mwanzinga Diwani wa Kata ya Matola

"Inabidi kama Halmashauri tuwe na orodha ya mafundi tuliofanya nao Kazi na wanaofanya Kazi nzuri.Ili wakiwa wanaomba Kazi tunaangia katika orodha yetu hii itatusaidia sana kuwa na miradi mizuri.Tusichukue fundi yeyote."Alisema Ultrick Msemwa Diwani wa Luponde

"Binafsi Nina orodha yangu ya mafundi ukiniuliza ntakwambia huyu ni mbabaishaji, huyu yupo taratibu lakini Kazi yake ni nzuri, huyu ni mzuri nakubaliana na Waheshimiwa Madiwani waliopita kuwa na orodha ya mafundi."Alisema Mbunge wa Jimbo la Njombe Mjini Deo Mwanyika

Baadhi ya Madiwani pia wamepongeza uongozi wa Kata ya Yakobi kwa jinsi wanavyofanya kazi kwa ushirikiano na wamesema kuwa kwa viongozi ambao wanashindwa kufanya kazi kwa pamoja wajifunze kupitia Yakobi.

"Shule ya Sekondari Yakobi Mkuu wa Shule ni Mwanamke,Mratibu Elimu Kata Mwnamke na Afisa Mtendaji kata Mwanamke.Kwa jinsi tulivyowaona ni kwamba wanafanya kazi kwa ushirkiano mkubwa tunawapongeza sana na huu ni mafno mzuri wa kuigwa."Alisema Mahenge Diwani wa Kata ya Mjimwema.

Halmashauri ya Mji Njombe kupitia mapato ya ndani na zidio la makusanyo imekuwa ikihakikisha kuwa miradi inayoibuliwa katika Vijiji na Mitaa inapatiwa fedha kigezo kikubwa ikiwa ni utayari wa Wananchi kuanzisha mradi na uchangiaji wao kwenye mradi husika mpaka kwenye hatua ya kuwa boma.







Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI,UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI. April 25, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA. December 20, 2024
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKUU WA WILAYA NJOMBE MHE. JUMA SWEDA ATOA WITO KUHUSU CHANJO YA PILI YA POLIO.

    April 29, 2025
  • AFISA MWANDIKISHAJI JIMBO LA NJOMBE MJINI AKUTANA NA VYAMA VYA SIASA

    April 24, 2025
  • ZIARA YA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA WILAYA YA NJOMBE KUKAGUA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    April 04, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Njombe awaonya wenyeviti kuhusu uharibifu wa miradi ya maendeleo

    February 15, 2025
  • Angalia zote

Video

WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI NA KUJITUMA
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe