• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

Miradi ya Kimkakati Njombe Yazivutia Halmashauri Nyingi Kujifunza

Tarehe iliyowekwa: October 28th, 2019

Ni ugeni uliohusisha Waheshimiwa  Madiwani na Wataalamu kutoka Manispaa ya Shinyanga ambapo walifika kwa lengo la  kujifunza kuhusu miradi mikakati ya stendi na soko inayotekelezwa na Halmashauri ya Mji Njombe ambapo gharama za miradi hiyo inakadiriwa kuwa bilioni 18 mpaka kukamilika kwake.

Akizungumza wakati wa kuukaribisha ugeni huo, Mkuu wa Wilaya ya Njombe Ruth Msafiri aliyekuwa ameambatana na Kamati ya Siasa ya Chama Cha Mapinduzi Wilaya ya Njombe, Mkuu wa Wilaya  amesema kuwa ni faraja kubwa kwa Wilaya yake kutembelewa  na ugeni huo kwani inadhihirisha wazi ni kwa namna gani miradi inayotekelezwa  katika Halmashauri imeakisi matamanio ya wengi na kuwa eneo la kujifunza.

“Tunaomba mtakaporudi mkawe mabalozi wetu. Yapo mengi ambayo mtakuwa mmejifunza kupitia ujenzi wa miradi ya soko na stendi. Kwa yale ambayo mtatushauri tupo tayari kupokea maboresho ili tuweze kufanya kazi vizuri zaidi.”Alisema Ruth Msafiri

Akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa miradi hiyo, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Njombe Illuminatha Mwenda alisema kuwa mikakati ya Halmashauri  ni kuhakikisha kuwa mapato yanakusanywa  kwa zaidi ya asilimia mia moja na ndipo lilipokuja wazo la kubuni miradi itakayoipatia Halmashauri mapato ya kudumu.

“Tunafahamu kuwa kupitia miradi hii tunatoa huduma kwa Wananchi lakini lengo letu kubwa kama Halmashauri ni kukusanya mapato. Ni vyema nanyi pia mkaona miradi ya namna gani mtakayoitekeleza itakayokuwa inatoa huduma kwa Wananchi na kama Halmashauri mkakusanya mapato.”Alisema Mwenda.

Akizungumza mara baada ya kutembelea kuona shughuli za ujenzi wa soko na kuona uendeshaji wa mradi wa stendi Naibu Meya wa Manispaa ya Shinyanga ameipongeza Halmashauri ya Mji Njombe kwa miradi iliyochaguliwa.

“Fedha ambayo imetumika kupitia miradi hii matokeo yake yanaonekana dhahiri. Miradi imetekelezwa kwa viwango vya hali ya juu na itaendelea kukuza kipato cha Wananchi wa Njombe.

Naye Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Njombe Edward Mgaya amewasihi Waheshimiwa Madiwani kuendelea kuwatumia wataalamu ipasavyo katika utekelezaji wa shughuli za maendeleo kwani mafanikio yanahitaji nguvu ya pamoja na busara katika kuelekezana ili kufikia maendeleo endelevu.

Ikumbukwe kuwa Halmashauri ya Mji Njombe kwa vipindi tofauti imekuwa ikipokea wageni kutoka Halmashauri mbalimbali kwa lengo la kujifunza na kubadilishana uzoefu.



















Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI,UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI. April 25, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA. December 20, 2024
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKUU WA WILAYA NJOMBE MHE. JUMA SWEDA ATOA WITO KUHUSU CHANJO YA PILI YA POLIO.

    April 29, 2025
  • AFISA MWANDIKISHAJI JIMBO LA NJOMBE MJINI AKUTANA NA VYAMA VYA SIASA

    April 24, 2025
  • ZIARA YA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA WILAYA YA NJOMBE KUKAGUA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    April 04, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Njombe awaonya wenyeviti kuhusu uharibifu wa miradi ya maendeleo

    February 15, 2025
  • Angalia zote

Video

WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI NA KUJITUMA
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe