• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

Njombe kuanzisha kiwanda cha kuchakata na kutengeneza plastiki

Tarehe iliyowekwa: April 4th, 2019

Halmashauri ya Mji Njombe kwa kushirikiana na Shirika la SHIPO ipo katika hatua za awali za kuanzisha kiwanda cha kuchakata  na kutengeneza bidhaa zitokanazo na plastiki, ambapo kwa mujibu wa takwimu jumla ya tani 1193 za plastiki huzalishwa kwa mwaka katika Halmashauri ya Mji Njombe na kupelekwa katika eneo la dampo kuu.

Akizungumza wakati wa kikao cha kupata maoni ya wadau juu ya mikakati na uboreshaji wa andiko la uanzishaji wa kiwanda hicho, ambapo kiliwashirikisha wadau wa Mazingira, Wachakataji wa bidhaa za plastiki kutoka Njombe, wataalamu kutoka Halmashauri na Shirika la SHIPO; Afisa Usafi na Mazingira Halmashauri ya Mji Njombe Nelson Mlwisa alisema kuwa Halmashauri kwa kushirikiana na SHIPO iliamua kuja na huo mkakati mara baada ya kuona ongezeko la uzalishaji taka za plastiki kwa mwaka na kiwanda hicho kitasaidia kuongeza thamani ya taka za plastiki na hivyo kupunguza taka zinazopelekwa dampo na kutoa fursa ya ajira kwa wakazi wa Njombe ikiwa ni katika zoezi la ukusanyaji, uchakataji, utengenezaji na uuzaji wa bidhaa zitokananzo na taka za plastiki.

Kwa upande wake mratibu wa miradi ya afya na usafi wa Mazingira kutoka SHIPO Eugenia Kimaro alisema kuwa kiwanda hicho kitatumia malighafi zitokazo nchini na elimu itatolewa kwa wale watakaokuwa tayari kupatiwa ujuzi wa uchakataji taka na utengenezaji bidhaa.

“Uzuri wa mradi huu ni kuwa mtashirikishwa kuanzia mwanzo mpaka mwisho. Wazawa mtashirikishwa kuanzia kipindi mashine zitakapoanza kutengenezwa, kufungwa, kufanya kazi na kwenye maboresho ya aina yoyote yale mtashirikishwa. Nyie wenyewe mtaimiliki teknolojia  na mtaweza kuiboresha kwa kadri itakavyowapendeza. Hii ina maana hata ikotokea SHIPO haipo leo, nyie mtakuwa tayari mnauwezo wa kutengeneza mashine hizi wenyewe na ndio maana tutatumia malighafi zitokanazo katika maeneo yetu hatutatumia vitu ambavyo ni vya gharama kubwa au vya nje kwani tunafahamu sio wote wenye uwezo wa kumudu gharama hizo” Alisema Kimaro

Vicent Kawogo Ni mmoja wa wadau wa uchakataji taka za plastiki kutoka Njombe, ambaye yeye alipongeza jitihada hizo za awali zilizofanywa na Halmashauri na Shirika la SHIPO na alisema kuwa kiwanda hicho kitakapokamilika kitawawezesha kupata soko la uhakika kwani kwa sasa mara baada ya kuchakata plastiki  hizo kuwa vipande vidogo vidogo wamekuwa wakizisafirisha kuzipelekea Dar es Salaam na ndipo husafirishwa kupelekewa India na China kwa ajli ya kutengeneza bidhaa za plastiki.

“Unaweza kuwa umesafirisha mzigo wako kupeleka Dar es Salaam ukifika pale unakuta kuna mabadiliko ya bei, bei iliyokuwa unaitegemea unakuta imeshuka na wewe umesafirisha kwa gharama kubwa kutoka Njombe mpaka Dar es Salaam hapo tayari umeingia hasara. Wakati mwingine unafika na mzigo unakuta kwa wakati huo India au China hawaitaji malighafi unaingia hasara nyingine. Kiwanda hiki kikikamilika inamaana hatutakuwa na usumbufu wa kusafirisha malighafi za plastiki kupeleka Dar es Salaam tutachakata na kutengeneza bidhaa za plastiki hapa Njombe na bei pia itakuwa ni nzuri kwani mlolongo wa upatikanaji bidhaa  unakuwa umepungua kwa kiasi kikubwa.”Kawogo alisema

Katika kufikia sera ya nchi ya uchumi wa viwanda jitihada mbalimbali zimekuwa zikifanyika kwa kushirikiana na wadau ili kuhakikisha kuwa Tanzania ya viwanda inafikiwa na Watanzania wanashiriki ipasavyo kwenye kufikia malengo haya.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI,UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI. April 25, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA. December 20, 2024
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKUU WA WILAYA NJOMBE MHE. JUMA SWEDA ATOA WITO KUHUSU CHANJO YA PILI YA POLIO.

    April 29, 2025
  • AFISA MWANDIKISHAJI JIMBO LA NJOMBE MJINI AKUTANA NA VYAMA VYA SIASA

    April 24, 2025
  • ZIARA YA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA WILAYA YA NJOMBE KUKAGUA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    April 04, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Njombe awaonya wenyeviti kuhusu uharibifu wa miradi ya maendeleo

    February 15, 2025
  • Angalia zote

Video

WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI NA KUJITUMA
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe