Kata ya Mokowo iliyopo kilomita 90 kutoka Mji wa Njombe ni miongoni mwa kata ambazo wananchi wake walikuwa na kiu ya kufikiwa na huduma mbalimbali ambazo zimewezekana katika kipindi cha miaka 4 ya Uongozi wa Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan .Miongoni mwa kazi kubwa zilizofanywa na Serikali katika kata hii ni pamoja na :Ujenzi wa kituo kipya cha Afya Makowo kwa gharama ya zaidi ya shilingi milioni 600,chenye vifaa tiba vya kisasa ikiwemo mashine ya kidijitali ya mionzi(X-Ray),gari jipya la wagonjwa na chumba chenye vifaa kwa jili kufanya upasuaji pamoja Ujenzi wa Shule mpya ya Sekondari Makowo kwa shilingi milioni 583 ambayo ilikuwa ni kilio cha wananchi cha muda mrefu.Halmashauri ya Mji Njombe tunasema asante wananchi wamefikiwa.
Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe