Shule mpya ya Msingi Lunyanywi itaongeza usalama kwa watoto na kuwapunguzia wanafunzi wanaotoka Lunyanywi na maeneo jirani zaidi ya km 9 za kutembea kuifuata elimu katika shule ya Msingi Mjimwema.
Mkuu wa Wilaya ya Njombe, Mhe. Juma Sweda, amewataka wafundi wanatekeleza mradi wa ujenzi wa bwalo la chakula katika shule ya Sekondari Yakobi kuhakikisha wanakamilisha kwa ubora uleule walioanza nao.Akizungumza Juni 18, 2025, wakati wa ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa bwalo hilo, Mhe. Sweda amepongeza ubora wa kazi iliyofanyika hadi sasa, ambapo zaidi ya shilingi milioni 169 kutoka mapato ya ndani ya Halmashauri zimeshatumika kutekeleza mradi huo ambao uko kwenye hatua za mwisho za ukamilishaji.
Mkuu wa Wilaya ya Njombe Mhe.Juma Sweda Juni 18,2025 alifanya ziara Halmashauri ya Mji Njombe na kukagua utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa matundu ya vyoo na mabweni katika shule ya Sekondari Matola,miradi inayotekelzwa kwa fedha zaidi ya Milioni 280 kutoka serikali kuu na mapato ya ndani ya Halmashauri.Katika ziara hiyo alipongeza juhudi zinazofanywa na Serikali kwa kutoa fedha zinazotumika kuboresha miundombinu mbalimbali kwenye sekta ya elimu na afya jambo ambalo linaondoa usumbufu kwa wananchi kuchangia shughuli za maendeleo.Katika kipindi cha miaka 5 ,zaidi ya shilingi Bilioni 1.5 zimetumika kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo kata ya Matola katika sekta ya Elimu na Afya.
Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe